• This page, Utawala wa Healey-Driscoll Wazindua Mpango wa Ruzuku ya Dola Milioni 14.3 kwa ajili ya Ukarabati katika Mipango ya Malezi ya Mtoto Zinazohudumia Familia zenye Kipato cha Chini, is   offered by
  • Department of Early Education and Care
Press Release

Press Release  Utawala wa Healey-Driscoll Wazindua Mpango wa Ruzuku ya Dola Milioni 14.3 kwa ajili ya Ukarabati katika Mipango ya Malezi ya Mtoto Zinazohudumia Familia zenye Kipato cha Chini

Kwa Mara ya Kwanza, Fursa za Mtaji Hutanguliza Miundombinu ya Kustahimili Hali ya Hewa na Kusisitiza Umuhimu wa Maboresho ya Usalama
For immediate release:
11/17/2023
  • Department of Early Education and Care

Media Contact   for Utawala wa Healey-Driscoll Wazindua Mpango wa Ruzuku ya Dola Milioni 14.3 kwa ajili ya Ukarabati katika Mipango ya Malezi ya Mtoto Zinazohudumia Familia zenye Kipato cha Chini

Alana Davidson, Director of Communications

BostonUtawala wa Healey-Driscoll ulitangaza leo kwamba Idara ya Elimu ya Mapema na Utunzaji (EEC) imefungua fursa za mtaji kwa ajili ya elimu ya mapema na vituo vya muda wa nje ya shule ambavyo vinahudumia familia zenye mapato ya chini.

Jumla ya ufadhili wa dola milioni 14.3 zinapatikana kusaidia ukarabati na miradi ya ujenzi ili kupanua uwezo na kuboresha ubora na ufikiaji wa mazingira ya kujifunzia kwa watoto, kuhakikisha wanakuwa na maeneo salama, jumuishi, na yanayofaa kimaendeleo ya kujifunza, kucheza na kukua. Kama sehemu ya mkabala wa serikali nzima wa Utawala wa kushughulikia matatizo ya hali ya hewa, EEC itatoa kipaumbele kwa miradi inayozingatia nishati safi na uondoaji kaboni. Miradi inayojumuisha kuboresha usalama ili kuzuia na kukabiliana na matishio yanayoweza kutokea kama vile timu ya wafyatuaji risasi na usakinishaji wa kamera za usalama na mifumo ya kudhibiti ufikiaji, pia itapewa kipaumbele.  

“Utawala wetu umejitolea kufanya elimu ya mapema na utunzaji kuwa nafuu zaidi na kuweka kufikiwa. Tunajivunia kuwa mpango huu wa mtaji huongeza ufadhili ili kuhakikisha kuwa mipango hii ina rasilimali za kifedha zinazohitajika kuwapa watoto wetu mazingira ya kisasa, mazuri na salama ya kujifunza na kucheza,” Gavana Maura Healey alisema. “Ruzuku hizi pia zitatusaidia kufanya maendeleo katika malengo yetu ya hali ya hewa, ambayo ni muhimu ili kuhakikisha watoto wetu wana maisha salama ya baadaye. Tunalishukuru Bunge kwa ushirikiano wao katika kupanua fursa za mtaji katika bajeti ya mwaka huu ili kuboresha na kupanua utoaji wa malezi ya watoto kwa wazazi walio na kipato cha chini, kusaidia uhamaji wao wa kiuchumi na kuimarisha uchumi wetu. 

“Uwekezaji huu wa dola milioni 14 katika miradi ya mitaji kwa ajili ya mipango ya elimu na matunzo ya watoto wachanga utasaidia kufanya jimbo letu liwe nafuu zaidi na lenye usawa, na kuunda aina za nafasi halisi za ndani na nje ambazo watoto wetu wanastahili kujifunza na kucheza kila siku,” Luteni Gavana Kim Driscoll alisema. “Fedha hizi zitaboresha ufanisi wa nishati ya mpango, uingizaji hewa na uhifadhi wa maji, upatikanaji wa familia na walimu katika mipango na maeneo ya nje ya michezo, kuunda madarasa mapya ya kuhudumia familia zetu zenye kipato cha chini, na mengi zaidi.”

“Massachusetts inaimarika zaidi tunapofanya kazi pamoja ili kutimiza malengo yetu, hasa inapohu susuala la sera ya hali ya hewa,” Mkuu wa Hali ya Hewa Melissa Hoffer alisema. “Uamuzi wa EEC wa kuweka kipaumbele miradi ya nishati safi na uondoaji kaboni kwa ruzuku hizi za mtaji na ni mfano mzuri wa mbinu yetu ya serikali nzima kutatua matatizo ya hali ya hewa. Ni muhimu kwamba tunajumuisha kwa makusudi hali ya hewa katika mambo yote tunayofanya ili Massachusetts iweze kulinda hali ya hewa ya siku zijazo kwa ajili ya kizazi kijacho.

Ruzuku hizi za mtaji wa elimu ya mapema zitaruhusu watoa huduma wa elimu ya mapema katika vituo vya huduma ya watoto wa familia kuboresha mazingira ambayo watoto hujifunza. Ruzuku hiyo huruhusu uboreshaji mbalimbali ikiwemo, lakini sio tu kwa, marekebisho ili kuboresha ubora wa hewa ya mazingira ya ndani, matengenezo ya dharura kama vile kubadilisha paa au kuboresha mifumo ya umeme au usalama, na marekebisho ya mazingira halisi ya kushughulikia ufikiaji au uboreshaji mwingine wa madarasa, maeneo ya nje, na zaidi. Miradi mikuu ya awali iliyoungwa mkono na EEC imeanzia kutoka njia za mwongozo hadi mifumo mipya ya usalama ya kadi ya ufunguo na kuongeza madarasa na bafu nyingi katika kituo.

Fursa za mtaji zinapatikana kupitia mseto wa vyanzo vya ufadhili, pamoja na milioni $6.8 milioni kutoka kwa Elimu ya Mapema na Ufadhili wa Muda wa Nje ya Shule (EEOST) kutoka FY24 ya Utawala - Mpango wa Uwekezaji wa Mtaji wa FY28 na $7.5 milioni za Mtaji wa Elimu ya Mapema na Mtoa Huduma, ufadhili uliotolewa katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2024. Ruzuku itatoa $200,000 - $500,000 kwa ajili ya ufadhili kwa kila mradi. Kwa mara ya kwanza, vituo vya kuwatunza watoto vya faida na mipango ya muda wa nje ya shule inayohudumia angalau 50% ya watoto wanaopokea usaidizi wa kifedha wa malezi ya watoto itastahiki kupitia maombi tofauti. Maombi ya miradi mikubwa inayofadhiliwa ($500,000 - $1,000,000 kwa kila mradi) yatapatikana kupitia EEOST yatapatikana hivi karibuni.

"Kwa kuweka fedha katika matengenezo, ukarabati na upanuzi katika vituo vya kulea watoto na vya mudai wa nje ya shule, tunaweza kuhakikisha kuwa wanafunzi wengi zaidi wanapata mazingira ya madarasa ambayo yanakuza masomo, ukuaji na uzoefu mzuri wa elimu,” Katibu wa Elimu Patrick Tutwiler alisema. “Ufadhili huu muhimu wa ruzuku utasaidia vituo vyetu vya kulea watoto na mashirika ya jamii katika kutoa nafasi zinazofikiwa, salama, na jumuishi kwa watoto wa jamii na uwezo wote, huku ukitusaidia kujenga maisha bora na endelevu ya siku zijazo.”

Utawala pia umefungua Ombi la Taarifa (RFI) ambalo linalenga kusaidia mipango ya malezi ya mtoto wa familia (FCC) kupitia ufadhili wa kujitolea wa mtaji, kuboresha ufikiaji sawa wa mtaji. EEC inatafuta maoni kuhusu njia bora ya kuwekeza fedha za mtaji katika biashara hizi ndogo ambazo zinaweza kuwasaidia kujenga utajiri na kuelekea kwenye umiliki wa mali, na pia kuunda fursa za kuunda mipango mpya ili kujenga ufikiaji mkubwa kwa familia. RFI pia inatafuta maoni kuhusu changamoto za kuanzisha biashara ya FCC na kupata leseni, na pia kuendesha na kuendeleza mipango ya ubora wa juu, ikijumuisha lakini sio tu kwa nafasi halisi, gharama za kuanza, mafunzo na sifa za kitaaluma, na uendeshaji wa biashara.

“Ninashukuru kwamba bajeti ya kihistoria ya jimbo ya EEC na kuongezeka kwa ufadhili katika Mpango wa mtaji wa Utawala kunatuwezesha kupanua fursa za mtaji katika elimu ya mapema na malezi, na pia kutafuta njia bora ya kusaidia mipango yetu ya malezi ya mtoto kwa familia kupitia ufadhili wa mtaji ambao hushughulikia mahitaji na changamoto zao za kipekee kama biashara ndogo ndogo,” Kamishna wa Elimu ya Mapema na Utunzaji Amy Kershaw alisema. “Uwekezaji huu wa dola milioni 14 utawawezesha watoto wetu, familia, na walimu kutumia wakati katika mazingira mapya zaidi, mazuri, endelevu na salama ya ubora wa juu, kusaidia familia kwenda au kurejea kazini na kujihusisha na elimu na mafunzo.”

“Mzunguko mdogo wa ruzuku wa mwaka huu utafungua fursa kwa watoa huduma wengi zaidi kuboresha vituo vyao. Tunashukuru kwa usaidizi thabiti wa Utawala wa uwekezaji wa mitaji kwa ajili ya malezi ya watoto. Kila mtoto anastahili mazingira ya mpango ambayo ni salama, yanayoboresha na kuchangia ukuaji chanya wa mtoto,” Theresa Jordan, Mkurugenzi, Hazina ya Uwekezaji wa Watoto alisema.

Fursa za mtaji zinasimamiwa na EEC kwa ushirikiano na Hazina ya Uwekezaji wa Watoto (CIF), mshirika wa Shirika la Usaidizi wa Maendeleo ya Kiuchumi ya Jamii (CEDAC). Maombi na RFI ilifunguliwa Novemba 9. Mawasilisho ya RFI yanastahili kuwasilishwa ifikiapo tarehe 15 Desemba. Maombi ya mtaji yatafungwa tarehe 23 Januari na kwa mara ya kwanza tutakubali saini ya kielektroniki na kujumuisha uwasilishaji kamili wa mtandaoni. Kuna vikao vya maelezo vinavyopatikana:

"Nafasi hizi za ruzuku ni mfano mwingine mzuri wa Marekebisho ya Haki ya Ushirikiano inayotekelezwa,” Seneta wa Jimbo Jason Lewis alisema, Mwenyekiti wa Seneti wa Kamati ya Pamoja ya Elimu. “Kwa usaidizi wa ziada kutoka kwa watu wanaopata mapato ya juu katika jimbo letu, tunaweza kuendelea kuwekeza katika elimu ya mapema ya hali ya juu, inayopatikana kwa wote, kupitia fursa za ruzuku kwa vituo vinavyohudumia familia zenye mapato ya chini. Kupitia ruzuku hizi, pia tunaendelea na dhamira yetu ya kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kukuza miundombinu ya nishati safi.

 “Ruzuku hizi zina jukumu muhimu katika kusaidia watoa huduma kutoa mazingira ambayo yanaakisi thamani ya elimu ya mapema na matunzo ya mtoto. Huu ni uwekezaji katika maeneo salama, yanayofaa na endelevu ili watoto wajifunze, kukua na kujiendeleza katika safari yao ya elimu,” Mwakilishi wa Jimbo Denise C. Garlick, Mwenyekiti wa Baraza la Kamati ya Pamoja ya Elimu alisema. 

###

Media Contact   for Utawala wa Healey-Driscoll Wazindua Mpango wa Ruzuku ya Dola Milioni 14.3 kwa ajili ya Ukarabati katika Mipango ya Malezi ya Mtoto Zinazohudumia Familia zenye Kipato cha Chini

  • Department of Early Education and Care 

    The Department of Early Education and Care's mission is to support the healthy growth and development of all children by providing high quality programs and resources for families and communities.
  • Help Us Improve Mass.gov  with your feedback

    Please do not include personal or contact information.
    Feedback